Jipime maarifa yako kuhusu twahara na swalah
Chemsha Bongo ya twahara na swalah 10
15:00
Imesuniwa kufanya nini kabla ya kuanza kuswali na viatu?
- Kuangalia chini kama vina najisi
- Kuvivua kabla ya kuanza kuswali
- Kuviweka ndani ya mfuko
Ni vipi vinasafishwa viatu vilivyo na najisi ili mtu aweze kuswali navyo?
- Kwa kutumia maji na sabuni
- Kwa kuvisugua chini kwenye ardhi
- Kwa kuvisugua na maji ya moto
Swalah ya kupatwa kwa jua ilitokea mara ngapi wakati wa Mtume?
- Mara 2
- Mara 1
- Haikutokea
Vipi Sujuud ya ambaye pua yake haikugusa ardhi?
- Sujuud yake haisihi
- Sujuud inasihi
- Sujuud yake inasihi tu kama ni swalah ya Sunnah
Ni lini mtu anazingatiwa amewahi Rakah katika swalah ya kupatwa kwa jua?
- Kwa kuwahi ile Rukuu´ ya kwanza ya Rak´ah ya kwanza
- Kwa kuwahi ile Rukuu' ya pili
- Anapojiunga na imamu kwenye Sujuud
Vipi wudhuu wa ambaye amegusa au amekanyaga kinyesi au mkojo?
- Bado yuko na wudhuu´ wake
- Wudhuu´ wake anaweza kuuswalia swalah za sunnah
- Umechenguka
Ni safari ya umbali kiasi gani inamruhusu msafiri kufupisha swalah yake?
- Ni ile ya umbali wa 50 km
- Ni ile ya umbali wa 40 km
- Sahihi ni kwamba ni ile ambayo watu wa maeneo yao wanaizingatia kuwa hiyo ni safari
Nini cha kufanya wakati mtu anatoa salamu wakati uko ndani ya swalah?
- Itikia kwa kuashiria kwa mkono tu
- Ni lazima kuitikia salamu kwa sauti
- Salamu inaitikiwa kama ni swalah ya faradhi
Ni vipi unasafishwa mkojo wa mtoto mchanga?
- Kwa kuosha na sabuni kama ni mkojo wa msichana
- Kwa kusugua na maji
- Kwa kurashia maji juu yake kama ni mkojo wa mtoto wa kiume ambaye hajaanza kula chakula
Kuna Dhikr maalum ya kusema kabla ya kuanza kuswali na kama ipo ni ipi?
- Ndio ipo, a´udhubillaahi mina shaytwaani rajiym
- Hakuna Dhikr yoyote maalum kabla ya swalah
- a´udhubillaahi mina shaytwaani rajiym bismillaahi Rahmaaniy Rahiym
Ni vipi inaondoshwa najisi iliyoingia kwenye nguo lakini hajui ni wapi?
- Kwa kuiosha pale unapodhani najisi imeingia
- Kwa kurashia maji juu yake
- Kwa kuiosha yote
Ni nini hukumu ya kuleta Qunuut katika swalah ya Fajr?
- Sunnah iliyosisitizwa
- Bid'ah
- Mtu ana khiyari akitaka afanye na akitaka aache
Ni ipi hukumu ya kusoma Aayah za Qur-aan za dua kwenye Sujuud?
- Haifai kabisa
- Inafaa kama ni kwa mtindo wa du'aa
- Akifanya hivo swalah inabatilika
Je, kuna swalah ya Sunnah kabla ya Maghrib?
- Ndio, Rak'ah 2 atakaye
- Hakuna ni Bid´ah
- Ndio, kuna Rak'ah 8 mtu anatakiwa kudumu nazo
Ni maeneo gani imesuniwa kwa mswaliji kukithirisha kuomba dua ndani ya swalah?
- Rukuu´
- Sujuud
- Anapoinuka kutoka kwenye Rukuu´
Ni kitu gani cha kwanza katika matendo ya waja Allaah atakifanyia hesabu siku ya Qiyaamah?
- Swawm
- Jihaad
- Swalah
Ni vipi inaondoshwa najisi iliyoingia kwenye ardhi?
- Kwa kusugua ardhi
- Kwa kurashia maji juu yake
- Kwa kumwagia maji mengi juu yake
Ni ipi hukumu ya msafiri anayeswali nyuma ya imamu mkazi?
- Lazima akamilishe swalah yake
- Anaweza kufupisha kwani ni msafiri
- Bora na Sunnah ni yeye afupishe swalah yake
Ni lini mtu anazingatiwa ameswali swalah ndani ya wakati wake?
- Akiwahi kuswali swalah kamili
- Akiwahi kuswali Rak'ah moja kamili
- Akiwahi dakika 10 kabla ya kumalizika wakati wake
Ni sehemu gani mswaliji anakuwa karibu zaidi na Mola wake ndani ya swalah?
- Kwenye Rukuu'
- Katika hatua zote
- Katika Sujuud
Ni vipi inaondoshwa najisi iliyoingia kwenye mkeka lakini hajui khasa ni wapi?
- Kwa kuuosha mkeka wote
- Kwa kuosha sehemu yake kubwa
- Kwa kurashia maji juu yake
Kama mtu amekosa Raatibah ya Fajr anaweza kuiswali lini?
- Imeshapita na hatoiswali
- Ataiswali baada ya swalah ya Fajr
- Ataiswali siku ya kufuata wakati wa Fajr