Qiyaamah hakitosimama ila kitawakumba waovu tu

Swali: Je, Qur-aan itapandishwa katika zama za mwisho?

Jibu: Ndio, wakati Qiyaamah kitaposimama. Wakati Qiyaamah kitaposimama Qur-aan itanyanyuliwa na wala hakutobaki katika ardhi mwenye kusema “Allaah! Allaah!”. Qiyaamah hakitosimama isipokuwa kitawakumba viumbe waovu ambao hawajui Dini na wala hawakatazi maovu, hawa ndio watasimamiwa na Qiyaamah na tunamuomba kinga kwa Allaah. Ama waumini zitachukuliwa nyoyo zao kabla ya hapo.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: http://www.alfawzan.af.org.sa/node/13537
  • Imechapishwa: 06/10/2020