Swali: Ni wajibu kumuitikia Salaam kafiri kama jinsi ni wajibu kumuitikia Muislamu?
Jibu: Ndio, huu ndio udhahiri wa Hadiyth. Amesema (Ta´ala):
وَإِذَا حُيِّيتُم بِتَحِيَّةٍ فَحَيُّوا بِأَحْسَنَ مِنْهَا أَوْ رُدُّوهَا
“Mtapoamkiwa kwa maamkizi yoyote, basi itikieni kwa yaliyo mazuri zaidi kuliko hayo au yarudisheni hayo hayo.” (07:86)
Hili ni kwa jumla.
Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Msianze kuwapa mayahudi na manaswara salamu. Endapo watakusalimieni itikieni:
“Wa ´alaykum.”[1]
Inatakiwa kuitikia wakitoa salamu. Udhahiri ni kwamba ni wajibu.
[1] Ibn Maajah (2999). Swahiyh kwa mujibu wa al-Albaaniy.
- Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh Qaa´idah Jaliylah fiyt-Tawassul wal-Wasiylah (03) http://www.alfawzan.af.org.sa/node/2106
- Imechapishwa: 01/07/2020
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket