Swali: Baada ya shahaadah mbili kuna upokezi unaosema kwamba mtu anatakiwa kusema:
“Na mimi nashuhudia kuwa kuwa hapana mungu wa haki isipokuwa Allaah. Nimeridhika na Allaah kama Mola…”?
Jibu: Hayo yanasemwa wakati wa shahaadah mbili, anatakiwa kusema mfano wake, kama alivyopokea Sa´d bin Abiy Waqqaaas:
“Mtu yeyote atakayesema wakati muadhini anaposema: ”Nashuhudia ya kuwa hakuna mungu wa haki isipokuwa Allaah…” kisha akasema: ”Nimeridhika na Allaah kuwa Mola wangu, Uislamu dini yangu na Muhammad Mtume wangu.”,
basi atasamehewa madhambi yake.”
Swali: Vipi kuhusu upokezi unaosema:
”Na mimi nashuhudia ya kuwa hapana mungu wa haki isipokuwa Allaah…”?
Jibu: Maana ni moja. Ni mamoja atasema:
“Nashuhudia…”
au:
“Nami nashuhudia… ”,
kwa sababu riwaya zimekuja kwa matamshi tofauti.
Swali: Lakini upande wa mapokezi ni Swahiyh?
Jibu: Dhahiri ni kwamba ni Swahiyh. Ikiwa mtu atasema:
“Nashuhudia ya kuwa hakuna mungu wa haki isipkuwa Allaah… ” au akasema “Na mimi nashuhudia ya kuwa hakuna mungu wa haki isipokuwa Allaah… ”,
basi atakuwa amesema mfano wake.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/27329/متى-يقال-وانا-اشهد-في-ترديد-الاذان
- Imechapishwa: 23/03/2025
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)