Swali 35: Tumesema kuhusu Hajj kwamba inafuta madhambi na anarudi mwenye kuhiji kama siku aliyozaliwa na mama yake. Hadiyth ambayo ndani yake Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alimwambia Swahabah ambaye aliweka sharti kwamba asamehewe yaliyopita, akamwambia:
”Je, hukujua kwamba Uislamu unafuta yaliyokuwa kabla yake na kwamba Hajj inafuta yaliyokuwa kabla yake?”
Je, katika hili kuna dalili kwamba hata madhambi makubwa pia husamehewa kwa kufanya Hajj?
Jibu: Dhahiri ya Hadiyth:
“Yeyote atakayehiji na asifanye upuuzi wala kufanya ufuska… ”
Ikiwa atatimiza kigezo hiki.
”… basi atarudi kutoka kwenye madhambi yake kama siku aliyozaliwa na mama yake.”[1]
Vilevile Hadiyth ya ´Amr bin al-´Aasw (Radhiya Allaahu ´anh) ambayo umeiashiria:
”Hakika Hajj inafuta yaliyokuwa kabla yake.”
dhahiri yake ni ujumla na hivyo inafuta kila kitu isipokuwa kufuru. Kwa hiyo ni lazima ndani yake kuwe na tawbah.
[1] al-Bukhaariy (1521) na Muslim (1350).
- Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (21/39-40)
- Imechapishwa: 25/05/2026
Swali 35: Tumesema kuhusu Hajj kwamba inafuta madhambi na anarudi mwenye kuhiji kama siku aliyozaliwa na mama yake. Hadiyth ambayo ndani yake Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alimwambia Swahabah ambaye aliweka sharti kwamba asamehewe yaliyopita, akamwambia:
”Je, hukujua kwamba Uislamu unafuta yaliyokuwa kabla yake na kwamba Hajj inafuta yaliyokuwa kabla yake?”
Je, katika hili kuna dalili kwamba hata madhambi makubwa pia husamehewa kwa kufanya Hajj?
Jibu: Dhahiri ya Hadiyth:
“Yeyote atakayehiji na asifanye upuuzi wala kufanya ufuska… ”
Ikiwa atatimiza kigezo hiki.
”… basi atarudi kutoka kwenye madhambi yake kama siku aliyozaliwa na mama yake.”[1]
Vilevile Hadiyth ya ´Amr bin al-´Aasw (Radhiya Allaahu ´anh) ambayo umeiashiria:
”Hakika Hajj inafuta yaliyokuwa kabla yake.”
dhahiri yake ni ujumla na hivyo inafuta kila kitu isipokuwa kufuru. Kwa hiyo ni lazima ndani yake kuwe na tawbah.
[1] al-Bukhaariy (1521) na Muslim (1350).
Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (21/39-40)
Imechapishwa: 25/05/2026
https://firqatunnajia.com/ni-lazima-hajj-aiambatane-na-tawbah-ya-kweli/