Swali: Ni ipi hukumu ya kutufu kwenye kaburi kama kaburi la al-Badawiy na mengineyo?
Jibu: Kutufu kwenye kaburi endapo mtu atanuia kujikurubisha kwa yule aliyemo ndani ya kaburi ni shirki. Twawaaf ni ´ibaadah ambayo anatakiwa kutekelezewa Allaah pekee. Amesema (Ta´ala):
وَلْيَطَّوَّفُوا بِالْبَيْتِ الْعَتِيقِ
“Watufu katika Nyumba kongwe.” (22:29)
Mwenye kutufu kinyume na Nyumba ya Allaah kwa lengo la kujikurubisha kwa mwengine asiyekuwa Yeye amemshirikisha Allaah. Amemfanyia ´ibaadah asiyekuwa Allaah. Twawaaf ni ´ibaadah kama mfano wa kuweka nadhiri, kuchinja na du´aa. Mwenye kumfanyia asiyekuwa Allaah ametumbukia kwenye shirki. Ni aina ya shirki kubwa.
- Muhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: http://www.alharamain.gov.sa/AudioDir2/67880.mp3
- Imechapishwa: 20/08/2017
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket