Swali: Ni ipi hukumu ya mwenye kusema:

“Msiwaraddi Ahl-us-Sunnah wenye kwenda kinyume ili kusiwepo mfarakano katika dini?”

Jibu: Kuraddi ni lazima. Lakini hata hivyo Radd zinafanywa na wanachuoni na wasomi. Vinginevyo ni lazima kuwaraddi wenye kwenda kinyume kwa ajili ya kubainisha uendaji kinyume waliyomo ili wengine wasije wakawaiga kichwa mchunga. Jingine ni kwamba huenda wakatubu kwa kwenda kwao kinyume. Lakini pamoja na hivyo hakuna wanaosimamia kazi hii isipokuwa wanachuoni.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Duruus-ul-Haram http://www.alfawzan.af.org.sa/node/14819
  • Imechapishwa: 28/06/2020