Swali: Mtu amejiunga katika swalah akiwa msafiri na akaswali nyuma ya imamu anayeswali swalah ya ´Aswr, hakuwahi isipokuwa Rak´ah mbili tu. Naye msafiri alikuwa amenuia kuswali kwa kufupisha. Akaswali Rak´ah hizo mbili pamoja na imamu kisha akasalimu pamoja naye. Ni ipi hukumu ya swalah yake?
Jibu: Msafiri akiswali nyuma ya mkazi huswali Rak´ah nne. Sunnah kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ni kwamba aswali Rak´ah nne akimfuata mkazi. Hivyo aliyewahi Rak´ah mbili za mwisho na akaziswali pamoja na mkazi, inamlazimu kuongezea Rak´ah mbili baada ya mkazi kusalimu ili kukamilisha nne. Yule ambaye hakufanya hivyo, basi inampasa kuirudia swalah aliyoswali Rak´ah mbili tu, kwa sababu kwake ni wajibu kuswali Rak´ah nne akiwa nyuma ya mkazi. Msafiri akiswali nyuma ya mkazi, huswali pamoja naye Rak´ah nne.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/31700/هل-يتم-المسافر-الصلاة-اذا-صلى-مسبوقا-مع-مقيم
- Imechapishwa: 15/11/2025
Swali: Mtu amejiunga katika swalah akiwa msafiri na akaswali nyuma ya imamu anayeswali swalah ya ´Aswr, hakuwahi isipokuwa Rak´ah mbili tu. Naye msafiri alikuwa amenuia kuswali kwa kufupisha. Akaswali Rak´ah hizo mbili pamoja na imamu kisha akasalimu pamoja naye. Ni ipi hukumu ya swalah yake?
Jibu: Msafiri akiswali nyuma ya mkazi huswali Rak´ah nne. Sunnah kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ni kwamba aswali Rak´ah nne akimfuata mkazi. Hivyo aliyewahi Rak´ah mbili za mwisho na akaziswali pamoja na mkazi, inamlazimu kuongezea Rak´ah mbili baada ya mkazi kusalimu ili kukamilisha nne. Yule ambaye hakufanya hivyo, basi inampasa kuirudia swalah aliyoswali Rak´ah mbili tu, kwa sababu kwake ni wajibu kuswali Rak´ah nne akiwa nyuma ya mkazi. Msafiri akiswali nyuma ya mkazi, huswali pamoja naye Rak´ah nne.
Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/31700/هل-يتم-المسافر-الصلاة-اذا-صلى-مسبوقا-مع-مقيم
Imechapishwa: 15/11/2025
https://firqatunnajia.com/msafiri-amemaliza-swalah-yake-baada-ya-kuwahi-rakah-mbili-nyuma-ya-mkazi/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket
