Msafiri aliyemkuta imamu ameshaswali Rak´ah mbili katika Dhuhr

Swali: Msafiri akimkuta imamu ambaye ni mkazi katika swalah ya Rak´ah nne naye akamkuta katika Tashahhud ya mwisho, je, ataswali Rak´ah mbili kisha amalize au aswali kwa kukamilisha?

Jibu: Anatakiwa aswali kwa kukamilisha. Akiunga pamoja naye, hata kama ni katika sehemu ya mwisho, anapaswa kukamilisha. Hilo ni kutokana na maneno yake Ibn ´Abbaas (Radhiya Allaahu ´anh):

“Kile mlichowahi kiswalini, na kile kilichowapita kikamilisheni.”

Kwa hiyo akiwahi pamoja naye Rak´ah moja, chini ya hapo au zaidi, anatakiwa aswali kwa kukamilisha.

  • Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (30/163)
  • Imechapishwa: 07/03/2026