Mgonjwa aliyevunjika mguu anaruhusiwa kukusanya swalah?

Swali: Ikiwa kuna mwanamke aliyevunjika mguu, je, inafaa kwake kukusanya swalah za nyakati mbili pamoja?

Jibu: Ikiwa anapata uzito katika kutawadha kwa kila wakati wa swalah mbili, basi inafaa kwake kukusanya swalah kama wagonjwa wengine. Ama ikiwa hakuna uzito, basi ataswali kila swalah katika wakati wake.

  • Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (30/178)
  • Imechapishwa: 09/03/2026