Swali: Maiti akifa usiku ni bora azikwe usiku huo au aachwe hadi asubuhi?

Jibu: Akipatwa na mauti mwanzoni mwa usiku, basi ni bora aswaliwe baada ya swalah ya Maghrib au ya ´Ishaa. Lakini akifa katikati ya usiku, kilicho bora zaidi ni kuchelewesha hadi aswaliwe baada ya swalah ya Fajr, ili watu wawe wengi zaidi katika kumhudhuria, kumsindikiza na kumwombea msamaha. Hilo ni bora kwake na kwa jamaa zake.

  • Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/1170/هل-يجوز-دفن-الميت-ليلا
  • Imechapishwa: 01/02/2026