Maana ya haki ya shahaadah

Swali: Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

“Nimeamrishwa kupigana vita na watu mpaka washuhudie ya kwamba ´hapana mwabudiwa wa haki isipokuwa Allaah na kwamba Muhammad ni Mtume wa Allaah`, wasimamishe swalah na watoe zakaah. Wakiyafanya hayo basi imesalimika kwangu damu na mali yao isipokuwa kwa haki yake na hesabu yao iko kwa Allaah (Ta´ala).” [1]

Nini maana ya kwa haki yake?

Jibu: Haki yake ni nguzo za Uislamu. Akikanusha kitu katika nguzo za Uislamu basi anapigwa vita. Ndio maana Abu Bakr as-Swiyddiyq (Radhiya Allaahu ´anh) aliwapiga vita wenye kukataa kutoa zakaah na akasema kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

”… isipokuwa kwa haki yake.”

na kwamba zakaah ni katika haki yake. Kwa maana nyingine ni katika haki ya shahaadah.

[1] al-Bukhaariy (25) na Muslim (22).

  • Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: ad-Durr an-Nadhwiyd (01)
  • Imechapishwa: 06/03/2025