Swali: Niliswali nyuma ya imamu swalah ya ´Aswr na nikasahau kusoma al-Faatihah katika Rak´ah ya kwanza. Je, imamu ananibebea nguzo hii?
Jibu: Ikiwa maamuma amesahau al-Faatihah au alikuwa hajui, basi imamu anambebea. Kama ilivyokuja katika Hadiyth ya Abu Bakrah ath-Thaqafiy (Radhiya Allaahu ´anh). Alikuja wakati imamu yuko katika Rukuu´, akarukuu kabla hajafika katika safu kisha akaingia katika safu. Akamuuliza Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ambaye alimwambia:
“Allaah akuzidishie pupa, lakini usirudie tena.”[1]
Hakumuamrisha kulipa Rak´ah ile, kwa sababu hakuhudhuria kisimamo chake.
[1] al-Bukhaariy (783).
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (30/157)
- Imechapishwa: 07/03/2026
Swali: Niliswali nyuma ya imamu swalah ya ´Aswr na nikasahau kusoma al-Faatihah katika Rak´ah ya kwanza. Je, imamu ananibebea nguzo hii?
Jibu: Ikiwa maamuma amesahau al-Faatihah au alikuwa hajui, basi imamu anambebea. Kama ilivyokuja katika Hadiyth ya Abu Bakrah ath-Thaqafiy (Radhiya Allaahu ´anh). Alikuja wakati imamu yuko katika Rukuu´, akarukuu kabla hajafika katika safu kisha akaingia katika safu. Akamuuliza Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ambaye alimwambia:
“Allaah akuzidishie pupa, lakini usirudie tena.”[1]
Hakumuamrisha kulipa Rak´ah ile, kwa sababu hakuhudhuria kisimamo chake.
[1] al-Bukhaariy (783).
Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (30/157)
Imechapishwa: 07/03/2026
https://firqatunnajia.com/maamuma-amesahau-kusoma-al-faatihah-katika-swalah-ya-kusoma-kimyakimya/