Ama kuhusiana na mashirika yanayofundisha, nasaha, kuamrisha mema, kukataza maovu na mambo mengine ambayo Uislamu umeweka, hatuyakemei.
Kwa kifupi tunakemea mashirika yanayoleta ukundi-ukundi, lakini hatukemei mashirika ambayo hayaleti ukundi-ukundi unaotenganisha Ummah katika makundi na mapote. Hakuna anayeweza kukataza shirika linalowafundisha watu Uislamu wa haki. Pengine umeona kuwa hakuna mgongano kwa yale niliyosema.
Swali: Nijuavyo ni kuwa makundi haya yamejifanya vyama-vyama.
Jibu: Mimi sikuzungumzia kuhusu kundi maalum na kama limewekwa katika Shari´ah au hapana. Ninasema kuwa kundi lolote lililojiweka vyama-vyama na shirika linalotoa bay´ah kwa kiongozi na mfano wa hayo husababisha tu Waislamu kufarikiana na kutofautiana.
- Muhusika: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Fataawaa Juddah (27)
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)