Swali: Baada ya mimi kuanza kumlingania mshirikina katika Uislamu na kuanza na Tawhiyd, nende naye hatua kwa hatua katika mambo mengine ya dini, kama kumkataza kunywa pombe na uzinzi, au nimwache kama alivyo mpaka pale moyo wake utapopata uimara juu ya Uislamu?

Jibu: Nenda naye hatua kwa hatua. Lakini hata hivyo usimkataze pombe na huku umemwacha juu ya shirki zake. Anza kwa shirki. Usimkataze pombe isipokuwa mpaka baada msimamo wake juu ya Tawhiyd uwe imara. Atapokuwa na uimara juu ya Tawhiyd ndio uende naye hatua kwa hatua na kumkataza maasi mengine. Anza kwa kitu muhimu zaidi.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh Fath-il-Majiyd (30) http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/fathul%20majd%20-%2019%20-%2010-%20-1436.mp3
  • Imechapishwa: 12/02/2017