Swali: Baadhi ya watu wa mashambani wanatoa Zakaat-ul-Fitwr nyama. Je, inajuzu?
Jibu: Haya si sahihi. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amefaradhisha Swaa´ ya chakula. Nyama inapimwa na wala haikadiriwi kwa kiasi. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amefaradhisha Swaa´ ya chakula. Ibn ´Umar (Radhiya Allaahu ´anhumaa) amesema:
“Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amefaradhisha Zakaat-ul-Fitwr Swaa´ ya tende au Swaa´ ya ngano.”
Sa´iyd al-Khudriy (Radhiya Allaahu ´anh) amesema:
“Tulikuwa wakati wa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) tukitoa Swaa´ ya chakula. Kipindi hicho chakula chetu kilikuwa ni tende, shayiri, zabibu na maziwa ya unga[1].”
Kwa ajili hii maoni sahihi ya wanachuoni ni kwamba si sahihi kutoa Zakaat-ul-Fitwr katika pesa, nguo au magodoro. Maoni yanayosema kuwa ni sahihi kutoa Zakaat-ul-Fitwr pesa hayazingatiwi. Midhali kuna dalili ya wazi kutoka kwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) hayachukuliwi maneno ya yeyote. Busara haina haki yoyote ya kuonelea uchaguzi fulani katika kubatilisha Shari´ah. Hapana shaka ya kwamba Zakaat-ul-Fitwr si sahihi isipokuwa katika chakula. Chakula chochote cha nchi ni sahihi kukitoa kama Zakaat-ul-Fitwr.
[1] Tazama https://en.wikipedia.org/wiki/Cottage_cheese
- Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (18/280-281)
- Imechapishwa: 23/06/2017
Swali: Baadhi ya watu wa mashambani wanatoa Zakaat-ul-Fitwr nyama. Je, inajuzu?
Jibu: Haya si sahihi. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amefaradhisha Swaa´ ya chakula. Nyama inapimwa na wala haikadiriwi kwa kiasi. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amefaradhisha Swaa´ ya chakula. Ibn ´Umar (Radhiya Allaahu ´anhumaa) amesema:
“Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amefaradhisha Zakaat-ul-Fitwr Swaa´ ya tende au Swaa´ ya ngano.”
Sa´iyd al-Khudriy (Radhiya Allaahu ´anh) amesema:
“Tulikuwa wakati wa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) tukitoa Swaa´ ya chakula. Kipindi hicho chakula chetu kilikuwa ni tende, shayiri, zabibu na maziwa ya unga[1].”
Kwa ajili hii maoni sahihi ya wanachuoni ni kwamba si sahihi kutoa Zakaat-ul-Fitwr katika pesa, nguo au magodoro. Maoni yanayosema kuwa ni sahihi kutoa Zakaat-ul-Fitwr pesa hayazingatiwi. Midhali kuna dalili ya wazi kutoka kwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) hayachukuliwi maneno ya yeyote. Busara haina haki yoyote ya kuonelea uchaguzi fulani katika kubatilisha Shari´ah. Hapana shaka ya kwamba Zakaat-ul-Fitwr si sahihi isipokuwa katika chakula. Chakula chochote cha nchi ni sahihi kukitoa kama Zakaat-ul-Fitwr.
[1] Tazama https://en.wikipedia.org/wiki/Cottage_cheese
Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (18/280-281)
Imechapishwa: 23/06/2017
https://firqatunnajia.com/kutoa-zakaat-ul-fitwr-nyama/
Mshirikishe mwenzako:
- Share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Print (Opens in new window) Print
- Email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Share on X (Opens in new window) X
- Share on Pocket (Opens in new window) Pocket