Swali: Je, ambaye anaswali, anafunga na anahiji lakini anawatembelea mawalii na anatafuta baraka kutoka kwao – mambo hayo yanaharibu matendo yake mema? Je, akifa anakuwa miongoni mwa watu wa Motoni?
Jibu: Kuhusu kuwatembelea mawalii na waislamu ni jambo limesuniwa. Bali inafaa kuyatembelea makaburi ya makafiri. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aliruhusiwa kumtembelea mama yake ambaye ni kafiri. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Nilikuwa nimewakatazeni kuyatembelea makaburi. Hivyo basi, yatembeleeni.”
Kuhusu kutafuta baraka, akiona kuwa maiti huyu anaathiri pamoja na Allaah au anaathiri badala ya Allaah, basi hiyo ni shirki. Asipoona kuwa ana uwezo wa kuathiri, basi kutafuta baraka kutoka kwake ni ukhurafi usiyofikia kiwango cha shirki.
- Muhusika: ´Allaamah Muqbil bin Haadiy al-Waadi´iy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Qam´-ul-Mu´aanid, uk. 27
- Imechapishwa: 16/02/2025
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)