Swali: Ni ipi hukumu ya mwenye kuingia msikiti ambao umetandikizwa sifongo juu yake? Ni ipi hukumu ya kusujudu juu ya vitu hivyo?
Jibu: Hakuna neno kuswali katika msikiti huu. Lakini anaposujudu abonyeze juu ya sifongo hiyo mpaka itulizane. Anas bin Maalik (Radhiya Allaahu ´anh) amesimulia:
“Tulikuwa tukiswali pamoja na Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Asipoweza mmoja wetu kumakinisha paji lake la uso juu ya ardhi, basi anatandaza nguo yake na anasujudu juu yake.”
Hii ni dalili inayoonyesha kwamba ni lazima kumakinisha paji la uso. Simaansihi kuwa umeweke kitu juu ya sifongo hiyo. Kwa sababu ukifanya hivo haitozingatiwa kuwa umesujudu. Kwa hivyo tunasema kwamba mtu akiswali msikitini au nyumbani kwake juu ya sifongo, basi ni lazima abonye juu yake mpaka itulizane.
- Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Liqaa’ ash-Shahriy (58) http://binothaimeen.net/content/1328
- Imechapishwa: 09/11/2019
Swali: Ni ipi hukumu ya mwenye kuingia msikiti ambao umetandikizwa sifongo juu yake? Ni ipi hukumu ya kusujudu juu ya vitu hivyo?
Jibu: Hakuna neno kuswali katika msikiti huu. Lakini anaposujudu abonyeze juu ya sifongo hiyo mpaka itulizane. Anas bin Maalik (Radhiya Allaahu ´anh) amesimulia:
“Tulikuwa tukiswali pamoja na Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Asipoweza mmoja wetu kumakinisha paji lake la uso juu ya ardhi, basi anatandaza nguo yake na anasujudu juu yake.”
Hii ni dalili inayoonyesha kwamba ni lazima kumakinisha paji la uso. Simaansihi kuwa umeweke kitu juu ya sifongo hiyo. Kwa sababu ukifanya hivo haitozingatiwa kuwa umesujudu. Kwa hivyo tunasema kwamba mtu akiswali msikitini au nyumbani kwake juu ya sifongo, basi ni lazima abonye juu yake mpaka itulizane.
Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: al-Liqaa’ ash-Shahriy (58) http://binothaimeen.net/content/1328
Imechapishwa: 09/11/2019
https://firqatunnajia.com/kusujudu-juu-ya-sifongo-godoro-dogo-au-kitu-mfano-wake/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)