Kuhusu upokezi wa Hishaam bin al-Ghaar kutoka kwa Mak-huul, ameitaja ´Abdullaah bin Sulaymaan kutoka kwa al-Ash´ath pasi na kuisikia kutoka kwake. Amesema:
86 – ´Abdullaah bin al-Isba´ al-Ba´lba´kiy ametuhadithia: al-Waliyd bin Muslim ametuhadithia: kutoka kwa Hishaam bin al-Ghaar, kutoka kwa Mak-huul, kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) Hadiyth mfano wa hii lakini hata hivyo yenyewe ni refu zaidi.
Ama kuhusu upokezi wa Ibn Abiy Hakiym kutoka kwa Mak-huul, ameeleza:
87 – Ahmad bin Muhammad bin Ziyaad ametuhadithia: al-Hasan bin ´Aliy bin Shabiyb ametuhadithia: Nilimsikia ´Amr bin ´Uthmaan akisema: Baqiyyah ametuhadithia: ´Utbah bin Abiy Hakiym ametuhadithia: Mak-huul amenihadithia: Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Allaah (´Azza wa Jall) hutazama katika kila usiku wa nusu Sha´baan ambapo akamsamehe kila mja isipokuwa mshirikina au mwenye chuki.”
- Muhusika: Imaam ´Aliy bin ´Umar ad-Daaraqutwniy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Kitaab-un-Nuzuul, uk. 167-168
- Imechapishwa: 09/05/2020
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket