78- Abu Ja´far Muhammad bin Sulaymaan bin Muhammad an-Nu´maaniy ametuhadithia: ´Abdullaah bin ´Abdis-Swamad bin Abiy Khidaa ametuhadithia: ´Iysaa bin Yuunus ametuhadithia, kutoka kwa al-Ahwas bin Hakiym, kutoka kwa Habiyb bin Suhayb, kutoka kwa Abu Tha´labah al-Khushaniy ambaye ameeleza kuwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Allaah (´Azza wa Jall) huwatazama waja Wake katika kila usiku wa nusu Sha´baan ambapo akawasamehe waumini, akawapa muhula makafiri na akawaacha wenye chuki na chuki zao mpaka waachane nazo.”[1]
[1] as-Sunnah (511) ya Ibn Abiy ´Aaswim. Shaykh al-Albaaniy amesema:
“Hadiyth ni Swahiyh na wapokezi wake ni waaminifu isipokuwa al-Ahwas bin Hakiym ambaye hifadhi yake ni nyonge, kama ilivyotajwa katika “at-Taqriyb”. Inaweza kutumiwa kwa lengo la shawahidi ambapo inatiliwa nguvu na njia zinazokuja mbele na mapokezi yaliyotangulia na mengine yatayotajwa.”
- Muhusika: Imaam ´Aliy bin ´Umar ad-Daaraqutwniy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Kitaab-un-Nuzuul, uk. 159-160
- Imechapishwa: 04/05/2020
- Taaliki: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket