21-  Abu Bakr an-Naysaabuuriy ametuhadithia: Ahmad bin Mansuur bin Raashid ametuhadithia: an-Nadhr bin Shumayl ametuhadithia: Muhammad bin ´Amr ametuhadithia, kutoka kwa Abu Salamah, kutoka kwa Abu Hurayrah ambaye amesimulia kuwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

“Allaah (´Azza wa Jall) anashuka kila usiku katika mbingu ya dunia kwenye nusu ya usiku au theluthi ya usiku na anasema mpaka alfajiri inaingia: “Ni nani aniombaye nimuitikie? Ni nani aniombae maghfirah nimghufurie? Ni nani aniulizaye nimpe?”

  • Mhusika: Imaam ´Aliy bin ´Umar ad-Daaraqutwniy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Kitaab-un-Nuzuul, uk. 105-106
  • Imechapishwa: 17/12/2019