Swali: Baadhi ya watu hulala wakati wa Khutbah ya ijumaa. Je, tukiwaamsha tutakuwa katika wale waliofanya upuuzi na hivyo hawana swalah ya ijumaa?

Jibu: Inapendekezwa kuwaamsha kwa kitendo, si kwa maneno. Kwa sababu kuzungumza wakati wa Khutbah hakujuzu. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

“Ukimwambia mwenzako ”Nyamaza!” siku ya ijumaa na imamu anakhutubu, basi umefanya upuuzi.”

Ameipokea al-Bukhaariy na Muslim.

Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alimuita huyo kuwa amefanya upuuzi ilihali anamwamrisha mema. Hilo linafahamisha wajibu wa kusikiliza kwa makini na uharamu wa kuzungumza wakati wa Khutbah.

  • Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (30/252)
  • Imechapishwa: 23/02/2026