Swali: Wakati kunasomwa Aayah inayomtaja Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ndani ya swalah – je, katika hali hiyo mswaliji amswalie Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam)?

Jibu: Ndio, kutokana na dhahiri ya maana ya Hadiyth. Isipokuwa wakati imamu anasoma kwa sauti ya juu. Katika hali hiyo anyamaze kwa ajili ya kisomo cha imamu. Lakini katika swalah ya kujitolea imamu asimame na aombe du´aa au amswalie. Vivyo hivyo afanye maamuma.

  • Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/29358/هل-يصلى-على-النبي-اثناء-الصلاة
  • Imechapishwa: 11/07/2025