Swali: Ni wajibu kwa mume kumhudumikia mkewe ambaye anafanya kazi kwa idhini yake?

Jibu: Ndio, hata kama atakuwa na mamilioni. Bado ni wajibu wa mume kumhudumikia. Hili halina shaka. Isipokuwa ikiwa kama alimshurutishia kuwa atajihudumikia mwenyewe. Waislamu wanatakiwa kutimiza masharti yao. Vinginevyo ni wajibu kwa mume kumhudumikia.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh Ighaathat-il-Lahfaan (37) http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/ighastah%20%20-%201%20-%2011%20-%201436.mp3
  • Imechapishwa: 13/02/2017