Kuitikia ”Ndio” katika Aayah ya mwisho ya Suurah al-Qiyaamah na at-Tiyn

Swali: Je inajuzu kusema “Ndio” katika Suurah zinazoishia kwa maswali, kama Aayah:

أَلَيْسَ اللَّـهُ بِأَحْكَمِ الْحَاكِمِينَ

”Je, kwani Allaah si Mwadilifu zaidi kuliko mahakimu wote?”[1]

na kama ilivyo kusema “Aamiyn” baada ya kusoma al-Faatihah?

Jibu: Ni jambo halikuwekwa katika Shari´ah isipokuwa wakati wa kusoma Aayah ya mwisho katika Suurah al-Qiyaamah, nayo ni maneno Yake (Ta´ala):

أَلَيْسَ ذَٰلِكَ بِقَادِرٍ عَلَىٰ أَن يُحْيِيَ الْمَوْتَىٰ

“Je, huyo hakuwa ni muweza wa kuhuisha wafu?”[2]

Inapendekezwa wakati wa kuisoma kusema:

سبحانك فبلى

“Kutakasika ni Kwako, ndio.”[3]

Kwa sababu Hadiyth imesihi juu ya hilo kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).

[1] 95:08

[2] 75:40

[3] Ahmad (7342) na Abu Daawuud (887).

  • Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (29/286)
  • Imechapishwa: 08/03/2026