Swali: Je, kuna ubora kufunga Muharram yote? Je, nakuwa mzushi kwa kufanya hivo?

Jibu: Baadhi ya wanazuoni wanasema kuwa ni Sunnah kufunga Muharram yote. Wanajengea hoja kwa maneno yake Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):

“Swawm bora baada ya Ramadhaan ni mwezi wa Allaah Muharram.”[1]

Hata hivyo kutokana na ninavojua ni kwamba haikupokelewa kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kwamba alifunga mwezi mzima. Mwezi unaofuata ambao Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa akifunga sana ni mwezi wa Sha´baan, kama ilivyopokelewa katika Hadiyth Swahiyh kutoka kwa ´Aaishah (Radhiya Allaahu ´anhaa)[2]. Wala haitakiwi kumtuhumu ambaye amefunga mwezi mzima, kwa sababu Hadiyth iliyotajwa inaweza kueleweka kwa njia hiyo, kama walivosema baadhi ya wanazuoni, kufunga mwezi mzima.

[1] Muslim (1163).

[2] al-Bukhaariy (1969) na Muslim (1156).

  • Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (20/22)
  • Imechapishwa: 19/03/2026