Tumeuliza kuhusu mtu ambaye anaandika yale anayosikia katika Khutbah ya ijumaa kwa sababu kuna watu wenye kusahau. Kwa hiyo akauliza kama inajuzu kuandika kila kunapopita sentesi yenye faida. Akijishughulisha na kuandika atapitwa na yaliyo baada yake. Binadamu hana mioyo miwili. Akijishughulisha na kuandika atapitwa na anayosema Khatwiyb wakati yuko anaandika.

Himdi zote ni Zake Allaah. Leo Allaah amejaalia kuwepo kwa vitu vyenye kurekodi. Unaweza kuleta kifaa cha kurekodi na ukarekodi Khutbah kwa starehe kisha ukaisikiliza nyumbani kwako, ndani ya gari lako na kwengineko.

  • Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh Riyaadh-is-Swaalihiyn (02/180-181)
  • Imechapishwa: 04/06/2024