Kile alichowahi mswaliji aliyekuja kuchelewa ndio sehemu yake ya mwanzo au ya mwisho?

Swali: Je, yale anayowahi mswaliji aliyekuja kuchelewa yanazingatiwa ndio ya sehemu yake ya mwanzo au sehemu yake ya mwisho?

Jibu: Maoni sahihi ni kwamba yale aliyowahi katika swalah yanazingatiwa ndio sehemu yake ya mwanzo na yale anayokidhi ndio sehemu yake ya mwisho. Kwa mfano akiwahi Rak´ah mbili za Dhuhr na akaweza kusoma Suurah nyingine baada ya al-Faatihah, atafanya hivo. Imamu anapotoa salamu, basi atasimama na kuswali Rak´ah zingine mbili na kusoma al-Faatihah peke yake. Kwa sababu yale anayokidhi ndio sehemu ya mwisho ya swalah yake. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

“Kile mlichowahi kiswalini, na kile kilichokupiteni kikamilisheni.”[1]

[1] al-Bukhaariy (636) na Muslim (602).

  • Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (12/447)
  • Imechapishwa: 12/04/2026