Swali: Allaah (Su:bhanaahu wa Ta´ala) amesema:

قُلْ هَلْ نُنَبِّئُكُمْ بِالْأَخْسَرِينَ أَعْمَالًا الَّذِينَ ضَلَّ سَعْيُهُمْ فِي الْحَيَاةِ الدُّنْيَا وَهُمْ يَحْسَبُونَ أَنَّهُمْ يُحْسِنُونَ صُنْعًا

“Sema: “Je, Tukujulisheni ni wepi ambao matendo yao yamekhasirika? Ni wale ambao wamepoteza juhudi zao katika uhai wa dunia nao wakidhani kwamba wanatenda vizuri.”[1]

Je, watu wa Bid´ah wanaingia ndani?

Jibu: Wana sehemu ya khasara. Hata hivyo khasara kamili ni ya washirikina makafiri. Ama mtu wa Bid´ah ni jambo linahitaji upambanuzi. Akifanya ukafiri basi yeye ni pamoja nao, na asipofikia ukafiri basi yuko katika khatari kutokana na Bid´ah yake.

Swali: Ni lini hayatajwi mazuri ya mzushi?

Jibu: Yule anayedhihirisha Bid´ah watu wanatahadharishwa kumhusu na mema yake hayawekwi wazi, kwa sababu makusudio ni kuwatahadharisha watu na shari, si kubainisha mema yake.

[1] 18:103-104

  • Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/31200/هل-يدخل-المبتدعة-في-وصف-الاخسرين-اعمالا
  • Imechapishwa: 13/10/2025