Swali: Kufanya ushabiki kwa madhehebu, kwa watu au kwa makundi kunahesabika kuwa ni aina ya kumuabudu asiyekuwa Allaah?

Jibu: Hapana, hayo ni maovu na haijuzu.

Swali: Je, hakuhesabiki kuwa ni katika kumwabudu asiyekuwa Allaah?

Jibu: Hapo ni pale mtu anapolihalalisha. Akiamini kuwa anayemfuata amekingwa na makosa na kwamba maneno yake yote ni ya haki, huko ni kuritadi. Ama kufuata kibubusa kwa jumla kunahitaji upambanuzi.

Swali: Baadhi yao wanasema:

“Kila jambo linalopingana na maneno ya imamu, basi linatakiwa kutafutiwa tafsiri.”

Jibu: Hayo ni kosa, linapaswa kukemewa bila shaka. Lazima kurejelea Maandiko na kuyaweka mbele ya kila kitu.

  • Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/31209/حكم-التعصب-للمذاهب-والاشخاص-والجماعات
  • Imechapishwa: 11/10/2025