Kalamu ndio kiumbe cha kwanza katika vile vinavyoonekana

Swali: Ni kipi kiumbe cha kwanza: kalamu au ´Arshi?

Jibu: Kiumbe cha kwanza kinachoonekana ni kalamu. Kuhusu viumbe kwa ujumla Allaah ndiye mjuzi zaidi. Wako wanazuoni waliosema kuwa ni ´Arshi. Maoni sahihi ni kwamba haitambuliki. Ibn-ul-Qayyim (Rahimhu Allaah) amesema:

Watu wametofautiana juu ya kalamu ambayo

makadirio yameitangulia kutoka kwa Hakimu

Je, ilikuwa kabla au baada ya ´Arshi?

kuna maono mawili kutoka kwa Abu ´Alaa´ al-Hamdaaniy

Sahihi ni kwamba ´Arshi ndio ilikuwa kabla

kwa sababu wakati wa uandishi ilikuwa na nguzo[1]

´Arshi ndio imeitangulia kalamu. Hata hivyo kalamu ndio kiumbe cha kwanza katika vinavyoonekana kama vile mbingu, ardhi n.k. Kwa sababu Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

“Allaah ameandika makadirio ya viumbe miaka 50.000 kabla ya kuumba mbingu na ardhi na ´Arshi Yake ilikuwa juu ya maji.”[2]

[1] an-Nuuniyyah.

[2] Muslim (2653).

  • Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh al-´Aqiydah al-Waasitwiyyah (01)
  • Imechapishwa: 13/05/2024