Kafara ya ambaye ameua watu wanne kwa gari

Swali: Nina ndugu yangu alipata ajali akiwa anaendesha gari na kosa lilikuwa lake kwa kuwa alikuwa na usingizi. Watu wanne walifariki kutokana na ajali hiyo. Je, juu yake kuna kafara nyingine zaidi ya kafara ya diyah na ni ipi?

Jibu: Yule aliyewapata watu kwa gari lake hali ya kuwa ana usingizi, si katika hali ya uangalifu kamili, juu yake kuna diyah na kafara. Yule aliyewagonga watu mpaka wakafariki, ni mamoja iwe ni kwa sababu ya kasi, usingizi, upungufu wa umakini au sababu nyingineyo, basi kwa hali yoyote amedhulumu na hivyo anawajibika diyah. Pia juu yake kuna kafara kwa kila nafsi; kafara yake ni kumuacha huru mtumwa. Akishindwa kufanya hivyo, basi afunge miezi miwili mfululizo kwa kila nafsi.

  • Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/1797/كفارة-من-قتل-بسيارته-وهو-نعسان
  • Imechapishwa: 19/12/2025