Swali: Je, inafaa kufuata kipofu katika mambo ya ´Aqiydah?
Jibu: Hapana. Kufata kichwa mchunga inakuwa katika mambo ya Fiqh kwa ambaye ni mjinga. Amesema (Ta´ala):
فَاسْأَلُواْ أَهْلَ الذِّكْرِ إِن كُنتُمْ لاَ تَعْلَمُونَ
“Basi waulizeni wenye ukumbusho kama nyinyi hamjui.”[1]
´Aqiydah hakuna kufuata kipofu. Ni lazima mtu ajifunze ´Aqiydah yake kwa mujibu wa Qur-aan na Sunnah na mfumo wa Salaf. Kuna vitabu vilivyothibitishwa, vidogo na vikubwa. Vipo vitabu vinavyobainisha ´Aqiydah ya Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah. Chukua kwa mfano “al-´Aqiydah al-Waasitwiyyah” ya Shaykh-ul-Islaam Ibn Taymiyyah (Rahimahu Allaah). Ni ´Aqiydah ilioenea inapokuja kubainisha ´Aqiydah na misingi ya Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah. Mfano wake ni “at-Twahaawiyyah” ya Imaam at-Twahaawiy na maelezo yake mnayosoma hivi sasa.
[1] 16:43
- Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh Fath-il-Majiyd (73)
- Imechapishwa: 09/04/2025
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)