Swali: Wako wenye kusema kuwa Ibliys hakukufuru kwa sababu alisema:
رَبِّ
”Mola!”[1]
فَبِعِزَّتِكَ
”Naapa kwa utukufu Wako.”[2]
Kwa msemo mwingine ni mwenye kutambua utukufu na ubwana wa Allaah.
Jibu: Ndio, ni mwenye kutambua Tawhiyd-ur-Rubuubiyyah. Abu Jahl na Abu Lahab, ambao ni makafiri na wataingia Motoni, walikuwa ni wenye kutambua Tawhiyd-ur-Rubuubiyyah kwa sababu walikuwa ni wenye kukanusha Tawhiyd-ul-Uluuhiyyah. Ibliys alikataa kutekeleza amri ya Mola wake. Alimwasi Mola wake na akafanya jeuri:
إِلَّا إِبْلِيسَ أَبَىٰ وَاسْتَكْبَرَ وَكَانَ مِنَ الْكَافِرِينَ
”… isipokuwa Ibliys alikataa na akatakabari na akawa miongoni mwa makafiri.”[3]
Tawhiyd-ur-Rubuubiyyah haitoshi na kusema tu:
رَبِّ
”Mola!”
فَبِعِزَّتِكَ
”Naapa kwa utukufu Wako.”
Hilo halitoshi. Ikiwa kweli kuna ambaye anasema kuwa Ibliys alikuwa muislamu basi ni msiba. Huo ni msiba.
[1] 15:31
[2] 38:82
[3] 02:34
- Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: http://alfawzan.ws/node/1875 Tarehe: 1431-04-14/2010-03-29
- Imechapishwa: 24/01/2021
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)