Swali: Ninajua watu wawili ambao walikuwa ni wapungufu katika kumtii Allaah (Ta´ala) na wakatoka na Jamaa´at-ut-Tabliygh na Allaah Akawastafidisha nao. Kwa hivyo,wakawa ni watendaji na wakaanza kutafuta elimu. Je, ni katika uadilifu kusema vibaya kikundi hichi?

Jibu: Ndio. Kikundi hichi ni Suufiyyah. Msingi wake ni Suufiyyah kutoka Pakistan. Bali miongoni mwao kuna waabudu makaburi kwa kuwa kinatokamana na Deoband. Deoband wengi wao ni waabudu makaburi. Ni kikundi ambacho hakiaminiki. Usiwe nao. Shikamaneni na watu wa Tawhiyd. Kikundi cha watu wa Tawhiyd katika mji huu wenye barakah himidi zote Zake Allaah. Wala msiangalie makundi yanayotoka huku na kule, na mifumo inayotoka huku na kule. Sisi tuko kwenye mfumo wa Qur-aan na Sunnah. Wajibu ni wao wastafidi kutoka kwetu na sio sisi kwao. Sisi mfumo wetu sio wa kimakosa. Mfumo wetu ni wa Tawhiyd na ´Aqiydah sahihi iliyojengeka juu ya Qur-aan na Sunnah na Da´wah sahihi. Wajibu ni wao kustafidi kutoka kwetu na sio sisi kustafidi kutoka kwao.

  • Mhusika: ´Allaamah Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: http://www.sahab.net/forums/index.php?showtopic=133508
  • Imechapishwa: 03/09/2020