Nilimuuliza Abu ´Abdillaah juu ya mtu ambaye baba yake amenyamaza kuhusu kuumbwa kwa Qur-aan. Akajibu:
“Amwamrishe na amfanyie upole.”
Nikamuuliza akiacha kuzungumza naye ikiwa atashikilia maoni yake. Akajibu:
“Ndio.”
Nikamuuliza Abu ´Abdillaah juu ya mtu ambaye dada yake au shangazi yake ameolewa na mtu ambaye amenyamaza juu ya uumbwaji wa Qur-aan. Akajibu:
“Akutane naye na amsalimie.”
Nikamuuliza ikiwa ni nyumba ya mwanamme huyo ambapo akajibu:
“Asimame nje ya mlango na asiingie ndani.”
- Muhusika: Imaam Muhammad bin Abiy Harb al-Jarjaara’iy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Masaa-il-ul-Imaam Ahmad, uk. 13-14
- Imechapishwa: 13/03/2021
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)