Swali: Je, inajuzu kwangu kutoa kiwango fulani cha pesa ili kuajiriwa kwangu kuweza kutimia pamoja na kuzingatia kwamba kupata kazi katika nchi yangu hakutimii isipokuwa kwa njia kama hii?
Jibu: Hapana. Hii ni rushwa. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amemlaani mwenye kutoa rushwa na yule mwenye kupokea. Ni haramu isiyojuzu. Milango ya riziki imefunguliwa. Tafuta riziki:
وَمَن يَتَّقِ اللَّـهَ يَجْعَل لَّهُ مَخْرَجًا وَيَرْزُقْهُ مِنْ حَيْثُ لَا يَحْتَسِبُ
“Na yule anayemcha Allaah humjaalia njia [ya kutokea] na atamruzuku kutoka njia ambayo hatizamii.”[1]
Riziki haipatikani kwa kuajiriwa peke yake.
[1] 65:02-03
- Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh ´Umdat-il-Fiqh (49)
- Imechapishwa: 29/01/2022
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)