Swali: Baadhi ya watu wanawakemea maimamu wa misikiti ambao wanasoma du´aa ya kukhitimu Qur-aan mwishoni wa mwezi wa Ramadhaan na wanasema kwamba ni jambo halikuthibiti kutoka kwa yeyote katika Salaf. Ni upi usahihi juu ya hilo?
Jibu: Hakuna ubaya kufanya hivo. Kwa sababu imethibiti kutoka kwa baadhi ya Salaf kwamba walifanya hivo. Jengine ni kwa sababu ni du´aa ambayo kumepatikana sababu yake katika swalah. Hivyo inaingia katika jumla ya du´aa za ndani ya swalah kama vile kukunuti katika Witr na wakati wa majanga.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (30/32)
- Imechapishwa: 21/05/2018
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)