Swali: Baadhi ya watu wanapohudhuria makaburini wanawakumbusha wahudhuriaji?

Jibu: Hapana vibaya. Ukumbusho hauna neno. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aliwanasihi watu walipokuwa makaburini wakisubiri kuzikwe. Akawanasihi kwa Hadiyth iliopokelewa na al-Bukhaariy na Muslim kupitia kwa al-Baraa´ bin ´Aazib na kwenye Sunan. Aliwanasihi walipokuwa wameketi wakisubiri.

Swali: Ukumbusho makaburi ni Sunnah au inapendeza tu?

Jibu: Inapendeza kutokana na kitendo chake Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).

  • Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/24585/هل-يستحب-تذكير-الحاضرين-في-المقبرة
  • Imechapishwa: 07/11/2024