Swali: Baadhi ya wanafunzi wanachukua minyororo ya wapokezi ya al-Bukhaariy na Muslim kwa ajili ya kuzisoma na kuzikosoa. Wanasema kwa mfano wanapotaja cheni ya al-Bukhaariy ya kwamba Hadiyth hii ni nzuri. Vivyo hivyo kuhusu Muslim.
Jibu: Maimamu wameafikina juu ya kuzikubali Hadiyth za ndani ya al-Bukhaariy na Muslim. Isipokuwa mambo machache ambayo al-Daraaqutwniy ameyakosoa ndani ya Muslim. Vinginevyo maimamu wameafikiana juu ya kukubali mapokezi ya al-Bukhaariy na Muslim na kwamba baada ya kuzidurusu na kuzipatiliza imebainika kusalimika kwake upande wa cheni zake. Watunzi wawili, al-Bukhaariy na Muslim, wamejitahidi katika hilo na kuzichagua kutoka katika mkusanyiko wa Hadiyth nyingi. Allaah awarehemu. Cheni zake ziko wazi.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/24617/هل-يوجد-خلاف-في-قبول-البخاري-ومسلم
- Imechapishwa: 14/11/2024
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)