Huu sio uitikiaji wa salamu

Swali: Vipi kwa yule ambaye anaposalimiwa husema:

أهلًا ومرحبًا

“Habari na karibu.”?

Jibu: Ni kwenda kinyume na Sunnah. Ni lazima aseme kama alivobainisha Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):

وعليك السلام ورحمة الله

“Nawe amani na rehema za Allaah ziwe juu yako.”

Lakini ni vizuri akizidisha baada yake, kama ambavo Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alifanya kwa Umm Haaniy´.

  • Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/24238/ما-حكم-رد-السلام-بقول-اهلا-ومرحبا
  • Imechapishwa: 20/09/2024