Swali: Kuna mtu amepitwa na swalah ya ´Aswr na alipokuja msikitini akakuta watu wameanza kuswali Maghrib. Je, aanze kuswali ile swalah iliyompita kabla ya Maghrib au hapana?
Jibu: Aswali Maghrib pamoja na imamu. Kisha aswali ´Aswr kwa maafikiano ya maimamu. Lakini je, arudi kuswali swalah ya Maghrib? Hakuna maoni mawili:
Ya kwanza: Airudi. Haya ni maoni ya Ibn ´Umar, Maalik, Abu Haniyfah na Ahmad katika maoni yaliyotangaa kwake.
Ya pili: Hatoirudi Maghrib. Haya ni maoni ya Ibn ´Abbaas, ash-Shaafi´iy na Hanaabilah katika maoni yao mengine.
Haya maoni ya pili ndio sahihi zaidi. Kwa sababu Allaah hakumuwajibishia mja kuswali swalah moja mara mbili midhali amemcha Allaah kiasi na uwezo wake – na Allaah ndiye mwenye kujua zaidi.
- Muhusika: Shaykh-ul-Islaam Ahmad bin Taymiyyah
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (22/106)
- Imechapishwa: 03/03/2019
Swali: Kuna mtu amepitwa na swalah ya ´Aswr na alipokuja msikitini akakuta watu wameanza kuswali Maghrib. Je, aanze kuswali ile swalah iliyompita kabla ya Maghrib au hapana?
Jibu: Aswali Maghrib pamoja na imamu. Kisha aswali ´Aswr kwa maafikiano ya maimamu. Lakini je, arudi kuswali swalah ya Maghrib? Hakuna maoni mawili:
Ya kwanza: Airudi. Haya ni maoni ya Ibn ´Umar, Maalik, Abu Haniyfah na Ahmad katika maoni yaliyotangaa kwake.
Ya pili: Hatoirudi Maghrib. Haya ni maoni ya Ibn ´Abbaas, ash-Shaafi´iy na Hanaabilah katika maoni yao mengine.
Haya maoni ya pili ndio sahihi zaidi. Kwa sababu Allaah hakumuwajibishia mja kuswali swalah moja mara mbili midhali amemcha Allaah kiasi na uwezo wake – na Allaah ndiye mwenye kujua zaidi.
Muhusika: Shaykh-ul-Islaam Ahmad bin Taymiyyah
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (22/106)
Imechapishwa: 03/03/2019
https://firqatunnajia.com/hukumu-ya-kuswali-maghrib-kabla-aswr-iliyompita-mtu/