Haitoshi kumuombea mtu maisha marefu tu

Swali: Je, du´aa ya kusema:

أمد الله عمرك

“Allaah aurefushe umri wako.”

au:

أطال الله عمرك

“Allaah akuze maisha yako.”

haifai kuombwa?

Jibu: Hapana, ikiwa ataongeza:

على خير

“… katika kheri.”

kama ilivyokuja katika Hadiyth ya kwanza, isipokuwa aweke sharti. Aseme:

“Allaah akurefushe umri katika kheri, katika uongofu, katika kutengemaa, katika Uislamu au maneno yanayofanana na hayo. Kwa sababu huenda Allaah akamrefushia umri katika shari.

  • Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/31649/ما-حكم-قول-اطال-الله-عمرك
  • Imechapishwa: 12/11/2025