Anamlazimisha mke kuwa na mafungamano mazuri na mamake

Swali: Mama yangu anamuudhi mke wangu na mimi niko ´Umrah. Namlazimisha mke wangu daima awe na mamangu. Je, nina haki kumlazimisha mke wangu kufanya hivo?

Jibu: Hapana, kuhusu kumlazimisha usimlazimishe. Lakini unachotakiwa ni kumuomba hili na kumpa moyo kumsaidia kumtendea wema mama yako na kwamba ana ujira katika kufanya hivo. Kuhusu kumlazimisha usimlazimishe.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Duruus-ul-Haram http://www.alfawzan.af.org.sa/node/14819
  • Imechapishwa: 28/06/2020