Amelipa deni lake la Ramadhaan siku ya mwisho ya Sha´baan kisha ikabaini kuwa siku hiyo ni Ramadhaan

Swali: Alikusudia kwa hilo kulipa siku aliyokuwa anadaiwa ya Ramadhaan ya mwaka uliopita. Baada ya kupita nusu ya mchana akapewa taarifa kuwa siku hiyo ni siku ya kwanza ya Ramadhaan. Je, swawm yake inatosheleza kuwa ni swawm ya siku ya kwanza ya Ramadhaan au haitoshelezi?

Jibu: Ana ujira wake – Allaah akitaka – lakini haisihi. Haitoshelezi wala kwa kulipa ile siku aliyokuwa anadaiwa na wala haitoshelezi kwa Ramadhaan. Haitoshelezi kwa kulipa deni lake, kwa sababu siku hiyo iliangukia ndani ya Ramadhaan. Wala haisihi kwa Ramadhaan, kwa sababu hakunuia swawm ya Ramadhaan. Matendo hutegemea nia. Basi juu yake ni kulipa siku hiyo tu.