Ameleta Takbiyr wakati wa kuinuka kutoka kwenye Rukuu´

Swali: Ni nini hukumu kwa imamu au maamuma akisema:

الله أكبر

”Allaah ni Mkubwa.”

badala ya kusema:

سمع الله لمن حمده

“Allaah amemsikia mwenye kumhimidi.”

au akasema kinyume chake?

Jibu: Haijuzu kufanya hivyo kwa makusudi. Wajibu kwa mwenye kuswali ni kuswali kama alivyokuwa akiswali Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Hivyo anatakiwa kuleta Takbiyr mahali pake, kusema:

ربنا ولك الحمد

“Mola wetu, himdi zote ni Zako.”

mahali pake, na kusema:

Yeyote atakayefanya kinyume cha hilo kwa kusahau, basi hana dhambi. Hata hivyo anatakiwa kuleta sijda ya kusahau ikiwa ni imamu au anaswali peke yake.

  • Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (29/290)
  • Imechapishwa: 06/03/2026