Ameapa kutouza bidhaa kwa chini ya pesa 100

Swali: Kuna mtu ameapa kwamba hatouza bidhaa fulani isipokuwa kwa pesa 100 ambapo akaiuza kwa pesa 90. Je, amevunja kiapo chake?

Jibu: Ndio. Akiapa kuwa hatoiuza isipokuwa kwa pesa 100 na akaiuza kwa chini ya hapo, amevunja kiapo chake. Lakini akiuza kwa thamani ya zaidi, hakuvunja kiapo chake.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh ´Umdat-il-Fiqh (42)
  • Imechapishwa: 28/06/2024