Swali 265: Ni yepi maoni yenye nguvu kuhusu kuweka mikono miwili baada ya kuinuka kutoka katika Rukuu´?
Jibu: Ni jambo sahali. Hakukuthibiti dalili sahihi na ya wazi kuhusu jambo hili. Kwa hivyo sisemi kuwa ni Bid´ah na wala sisemi pia kuwa ni Sunnah. Lakini hata hivyo ni jambo la ki-Ijtihaad. Mwenye kuweka mkono wake wa kuume juu ya mkono wake wa kushoto juu ya kifua baada ya kuinuka kutoka katika Rukuu´ ametendea kazi yale yaliyoenea. Na vilevile mwenye kuachia mikono ametendea kazi Hadiyth ilioko katika “as-Swahiyh” ya Muslim.
- Muhusika: ´Allaamah Muqbil bin Haadiy al-Waadi´iy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Ijaabatu as-Saa-il, uk. 500
- Imechapishwa: 29/11/2019
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket