Shaykh-ul-Islaam Ibn Taymiyyah amesema:
Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alisema kumwambia kijakazi:
“Allaah yuko wapi?” Akajibu: “Juu mbinguni.” Akamuuliza tena: “Mimi ni nani?” Akajibu: “Wewe ni Mtume wa Allaah.” Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akasema: “Mwache huru. Kwani hakika ni muumini.”[1]
MAELEZO
Mu´aawiyah bin al-Hakam as-Sulamiy alighadhibika ambapo akampiga kofi kijakazi wake. Kisha akajuta kwa kumpiga na akataka kutoa kafara juu ya kitendo chake. Hivyo akataka kumwacha huru na akaenda kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kumuuliza juu ya jambo hilo. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akamjaribu na kumuuliza:
“Allaah yuko wapi?” Akajibu: “Juu mbinguni.” Akamuuliza tena: “Mimi ni nani?” Akajibu: “Wewe ni Mtume wa Allaah.” Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akasema: “Mwache huru. Kwani hakika ni muumini.”
Wakati alipojibu kuwa Allaah yuko juu ya mbingu, ndipo (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akamthibitishia imani. Hapa kuna faida kubwa:
1 – Inafaa kuuliza ni wapi yuko Allaah, kwa sababu Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alisema:
“Allaah yuko wapi?”
Bi maana upande gani. Swali hili linafaa na ni jambo ambalo mjinga anatakiwa kufunzwa.
2 – Anayemsifu Allaah kuwa juu ni muumini, na asiyemthibitishia Allaah (´Azza wa Jall) kuwepo juu ya mbingu ni kafiri. Hakuna Hadiyth ambayo ni pigo kwa Mu´tazilah kama hii. Wao wanaona kuwa haifai kuuliza ni wapi alipo Allaah. Kwa sababu wao wanaona kuwa Allaah yuko kila mahali au kwamba hana mahali; hayuko ndani, wala nje, wala kualini, wala kushotoni na kadhalika. Kwa msemo mwingine Hapatikani.
[1] Muslim (537), Abu Daawuud (930), an-Nasaa’iy (3/13), Maalik (2/776), Ibn Abiy ´Aaswim (479), al-Bayhaqiy, uk. 422, Ahmad (5/447) na Abu Daawuud at-Twayaalisiy (1105).
- Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: at-Ta´liyqaat at-Tawdhwiyhiyyah ´alaa Muqaddimat-il-Fatwaa al-Hamawiyyah, uk. 126-127
- Imechapishwa: 26/08/2024
Shaykh-ul-Islaam Ibn Taymiyyah amesema:
Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alisema kumwambia kijakazi:
“Allaah yuko wapi?” Akajibu: “Juu mbinguni.” Akamuuliza tena: “Mimi ni nani?” Akajibu: “Wewe ni Mtume wa Allaah.” Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akasema: “Mwache huru. Kwani hakika ni muumini.”[1]
MAELEZO
Mu´aawiyah bin al-Hakam as-Sulamiy alighadhibika ambapo akampiga kofi kijakazi wake. Kisha akajuta kwa kumpiga na akataka kutoa kafara juu ya kitendo chake. Hivyo akataka kumwacha huru na akaenda kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kumuuliza juu ya jambo hilo. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akamjaribu na kumuuliza:
“Allaah yuko wapi?” Akajibu: “Juu mbinguni.” Akamuuliza tena: “Mimi ni nani?” Akajibu: “Wewe ni Mtume wa Allaah.” Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akasema: “Mwache huru. Kwani hakika ni muumini.”
Wakati alipojibu kuwa Allaah yuko juu ya mbingu, ndipo (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akamthibitishia imani. Hapa kuna faida kubwa:
1 – Inafaa kuuliza ni wapi yuko Allaah, kwa sababu Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alisema:
“Allaah yuko wapi?”
Bi maana upande gani. Swali hili linafaa na ni jambo ambalo mjinga anatakiwa kufunzwa.
2 – Anayemsifu Allaah kuwa juu ni muumini, na asiyemthibitishia Allaah (´Azza wa Jall) kuwepo juu ya mbingu ni kafiri. Hakuna Hadiyth ambayo ni pigo kwa Mu´tazilah kama hii. Wao wanaona kuwa haifai kuuliza ni wapi alipo Allaah. Kwa sababu wao wanaona kuwa Allaah yuko kila mahali au kwamba hana mahali; hayuko ndani, wala nje, wala kualini, wala kushotoni na kadhalika. Kwa msemo mwingine Hapatikani.
[1] Muslim (537), Abu Daawuud (930), an-Nasaa’iy (3/13), Maalik (2/776), Ibn Abiy ´Aaswim (479), al-Bayhaqiy, uk. 422, Ahmad (5/447) na Abu Daawuud at-Twayaalisiy (1105).
Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: at-Ta´liyqaat at-Tawdhwiyhiyyah ´alaa Muqaddimat-il-Fatwaa al-Hamawiyyah, uk. 126-127
Imechapishwa: 26/08/2024
https://firqatunnajia.com/86-hakuna-hadiyth-ambayo-ni-pigo-kwao-kama-hadiyth-ya-kijakazi/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)