Swali 67: Baadhi ya vitanda vya majeneza vinawekwa kalima ya Tawhiyd. Ni ipi hukumu yake[1]?
Jibu: Hili ni jambo halikuwekwa katika Shari´ah. Kilichowekwa katika Shari´ah ni kumtamkisha shahaadah ambaye anataka kukata roho. Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Watamkisheni maiti wenu ´Laa ilaaha illa Allaah´.”
Ameipokea Muslim.
Makusudio ya maiti hapa ni wale wanaotaka kukata roho mpaka neno lao la mwisho liwe “Laa ilaaha illa Allaah”.
Kuhusu kuandika juu ya sanda au kaburi lake haijuzu.
[1] Majmuu´-ul-Fataawaa (13/186).
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Ahkaam-ul-Janaa-iz, uk. 51
- Imechapishwa: 29/12/2021
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)